Lebo

Jumapili, 28 Juni 2015

Watu wawili wauawa siku 1 kabla ya uchaguzi nchini Burundi

 
Watu 2 wameuawa Burundi katika mashambulizi ya gruneti na ufyatulianaji risasi katika ngome za upinzani katika mji mkuu wa Bujumbura siku moja kabla ya uchaguzi wa wabunge.
Uchaguzi huo ambao umekumbwa na utata baada ya makundi ya upinzani kuandamana na ilikupinga hatua ya rais Pierre Nkurunziza kuwania muhula wa tatu.
Upinzani unadai kuwa rais Nkurunziza anakiuka katiba ya taifa na mapatano ya Arusha yalyokomesha vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Walioshuhudia mauaji hayo wanawalaumu polisi kwa mashambulizi na vifo hivyo vilivyotokea katika maeneo ya mji mkuu wa Bujumbura ambayo yanadhaniwa kuwa ni ngome ya vyama vya upinzani.
Jumamosi watu waliokuwa wamejihami na bunduki walivamia kituo cha kuhifadhia makaratasi ya kupigia kura na kuyachoma moto.

Tukio hilo lililotokea Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo iliwaacha wengi vinywa wazi wasijue waliotekeleza mashambulizi hayo ni kina nani wala nia yao ilikuwa nini.Burundi imekumbwa na mzozo wa kisaisa tangu rais Nkurunziza atangaze nia ya kuwania muhula wa tatu.
 null
Upinzani umekuwa ukiandaa maandamano mjini Bujumbura ilikumshinikiza ajiondoe katika kinyang'anyiro hicho.
CHANZO:BBC SWAHILI

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni