Pamoja na mambo mengine yaliyozungumzwa na Mhe.Zitto Ayatollah Kabwe katika hotuba yake katika viwanja vya Mwembeyanga hapo jana ni kuhusu Watanzania walioficha fedha nchini Uswisi. Kutoka mwaka 2012 ilipotoka ripoti ya bunge ya kuitaka serikali kuchunguza majina ya Watanzania walioficha fedha nje ya nchi, kulikuwa na hoja kubwa mbili ambazo hazijathibitishwa kwa namna yoyote ile na kile kinachoitwa Zitto kuwataja majina Watanzania walioficha hela nje ya nchi.
Awali ya yote ieleweke wazi kuwa si dhambi kwa Mtanzania kuwekeza au kuhifadhi fedha nje ya nchi hivyo hoja ni sifa na uhalali wa fedha hizo. Kwa muktadha huo kile kichokuwa kinatizamwa kwa kipindi kirefu ni aidha fedha hizo ni umma na zimefanyiwa mchezo wa kifisadi na baadhi ya watendaji waandamizi wa serikali walioamua kwenda kuficha fedha hizo nje ya nchi ili kijinasua na uchunguzi wa tume ya maadili ya viongozi wa umma au usalama wa taifa (TISS). Pili, hoja kubwa ilikuwa kwamba fedha hizo ni faida ya uhujumu uchumi miongoni mwa Watanzania jambo ambalo Mhe.Zitto Kabwe ameshindwa kutueleza. Rejea aya hii iliyopo katika hotuba yake:
"Fedha hizi zaweza kuwa halali ama haramu. Kuna watu ama ni Watanzania wanaishi ughaibuni na kufanya kazi huko ni lazima wawe na akaunti za benki. Pia kuna Watanzania ambao ni wafanyabiashara na masharti ya biashara zao ni lazima wawe na akaunti katika mabenki ya nje. Hata hivyo mfumo mzima wa ufunguaji na ufungaji wa akaunti katika mabenki ya nje umewekewa masharti ya kisheria na kibali cha Benki Kuu kinahitajika. Kuna Watanzania wenye kuficha fedha ambazo zimepatikana kwa rushwa na biashara haramu mbalimbali kama vile madawa ya kulevya na biashara ya nje ambayo haingii kwenye rekodi za Benki Kuu. Iwapo Serikali ingefanya uchunguzi na kuukamilisha tungeweza kujua kwa hakika katika orodha ya watu wenye akaunti nje ni wepi wana fedha zao halali na wepi wana fedha haramu. Serikali imetunyima haki hiyo kwa zaidi ya miaka miwili na nusu sasa. Bunge la Kumi linavunjwa mnamo tarehe 9 Julai mwaka huu na hakuna dalili yeyote ya Serikali kutoa taarifa ya uchunguzi ndani ya bunge kama ilivyoagizwa na Bunge."
Kumbe alichokifanya Mhe.Zitto ni kuendeleza maisha ya tetesi badala ya kuutafuta ukweli. Toka mwaka 2012 alitakiwa kuwataja wahusika lakini akafyata mkia, je alisubiri zibaki siku 5 za kulivunja bunge ndipo awataje wahusika?
Pia jambo linalotia wasiwasi ni majina ya watajwa, je hakuna Watanzania wengine nje ya wenye majina ya kiarabu na kihindi?
Tatu, uhalali wa majina hayo ni upi maana hayaeleweki yametoka taasisi gani ya kiuchunguzi ama benki husika ili tuamini kuwa ni ya kweli, vile vile TAKUKURU na TISS wapate msaada wa kuutafuta ukweli?
Nne, kwanini Mhe.Zitto Ayatollah asisome mwenyewe majina hayo ili awe sehemu ya ushahidi kama alivyowataja Dr.Willbrod Slaa katika List Of Shame, badala yake Zitto akawapa waandishi majina ambayo si tu kwamba yanamuweka mbali na ushahidi bali pia hayana sahihi yake. Kwa ujumla majina yaliyotajwa na Mhe.Ayatollah kama ambavyo wachambuzi wengi wamechambua, hayajatibu kiu ya watanzania waliotaka kufahamu ukweli wa jambo hili. Zitto anatakiwa kujipanga upya vinginevyo umma utazidi kupoteza imani kwa mwenendo wa siasa za aina hii.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni