![]() |
Waziri mkuu wa zamani Uganda Amama Mbabazi |
Siku ya Jumatano Polisi nchini Uganda walitoa taarifa kusema kuwa bwana Mbabazi hana ruhusa ya kufanya mikutano yoyote ya kisiasa japo alikuwa amewataarifu.
Bwana Mbabazi ananuia kutafuta uteuzi wa chama kinachotawala NRM kuwa mgombea wake rasmi wa Urais katika uchaguzi huo Machi mwaka ujao.
![]() | |
Dr. Kizza Besigye |
Alikamatwa akiwa njiani kwenda kwenye mkutano wake wa kwanza na wafuasi wa chama chake cha Forum For Democratic Change.
Msaidizi wa Dr Besigye ameiambia BBC kuwa mwanasiasa huyo anazuiliwa katika kituo cha polisi karibu na nyumbani kwake. Besigye anashindania kiti hicho cha FDC na aliyekuwa kamanda wa jeshi Gen. Mugisha Muntu.
Dr. Besigye pamoja na bwana Mbabazi wote walikuwa washirika wa karibu zaidi na rais Yowei Museveni ambaye atashindana nao katik auchagzui huo.Museveni amekuwa uongozini kwa miaka thelathini.
Kwa sasa #FreeBesigye inaendelea kutajwa kwa wingi katika mitandao ya kijamii, baada ya watu kugeukia mitandao hiyo kuelezea hisia zao kuhusu kukamatwa kwa wawili hao.
SOURCE:BBC Swahili
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni