![]() |
Katibu Mkuu wa CCM, Mhe. Kinana akipanda boda boda ya askari polisi |
Ni kweli mara kadhaa Mhe.Kinana ameonekana runingani akichezea matope sawa na waashi, amewahi kuonekana kwenye mashamba ya chai akiigiza kuchuma chai n.k lakini hapo alipofika kwa askari wetu wanaolipwa kodi za wananchi wa vyama vyote halafu anajengewa taswira kuwa mwanachama wa CCM, hii haivumiliki.
Ni mara nyingi jeshi la polisi limetuhumiwa na vyama vya upinzani kwamba linakipendelea chama tawala, tuhuma zimekanushwa mara nyingi lakini kwa hiki kitendo cha Mhe. Kinana lazima kikemewe. Ni vigumu kuamini kwamba askari huyo pichani hakufunzwa kwamba hastahili kuwa shabiki wa chama chochote, wala asishiriki siasa zaidi ya kupiga kura tu?
Hivi Mhe.Kinana anataka tuamini kwamba hajui waraka namba 1 wa mkuu wa utumishi wa umma unasema nini kuhusu watumishi wa umma kutokushiriki siasa? Ngoja nimkumbushe yeye na watumishi wengine wa umma sambamba na wanasiasa wanaopenda sifa zisizostahili sambamba na siasa zinazoweza kuchochea ghasia.
JAMHURl YA MUUNGANO
WA TANZANIA
OFISI VA RAIS IKULU,
S.L.P 9120,
DAR-ES-SALAAM. Kumb. Na. SHCIC.180/2/113 26 Juni, 2000
WARAKA WA MKUU WA UTUMISHI WA UMMA
NA. 1 'WA MWAKA 2000
KUHUSU MAADILI
YA WATUMISHI WA UMMA KATlKA MFUMO WA VYAMA VINGI VYA
SIASA
1.0 UTANGULIZI:
1.1 Kuanzia mwaka 1965
hadi 1992
Tanzania ilipokuwa na Mfumo wa Siasa
wa Chama Kimoja
Watumishi wote wa Serikali na Vyombo vyake
siyo tu waliruhusiwa bali ilionekana ni wajibu
wao kushiriki katika mambo ya kisiasa. Shughuli nyingi za kiserikali na za kisiasa zilikwenda kwa pamoj ana palikuwepo na maingiliano makubwa
kati ya sehemu hizi mbili katika shughuli zote za kiutendaji, kiuongozi
na kiitikadi.
1.2 Kufuatia mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tan-
zania yaliyofanyika Julai, 1992 na kuruhusu
mfumo
wa vyama vingi vya siasa,
Serikali ilitoa maelekezo ya jinsi
watumishi
watakavyoshiriki katika
mambo yaSiasa kupitia Waraka wa Mkuu wa Utumishi
wa Umma Na. 1 wa Mwaka
1992.
1
2.0 UTARATIBU
ULIOTOLEWA KATlKA
WARAKA
WA MKUU WA UTUMISHI WA UMMANA.1
WAMWAKA
1992:
Utaratibu uliotolewa katika Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Na. 1 wa Mwaka 1992
uliwagawa watumishi wa umma
katika makundi mawili
na
kuweka Masharti ya
namna watakavyoshiriki katika Siasa.
2.1
Watumishi
wa Kundi "A" walijumuisha Watumishi wa ngazi zajuu
Serikalini, Serikali za Mitaa
na katika
Mashirika ya Umma wanaoshughulikia uandaaji
11a
usimamizi wa sera. Hawa ni watumishi waandamizi wenye
Madaraka kuanzia ngazi
ya Mkurugenzi na kuendelea juu,
Meneja Msaidizi na kuendelea juu na
ngazi ya Mkurugenzi Mtendaji.
Nikienda moja kwa moja kwenye kifungu lengwa:
3.3 Mbali ya makundi yaliyotajwa katika aya ya 2 hapa juu kuna makundi
ya watumishi wa umma ambao hawakuorodheshwa katika
Waraka huo lakini kwa mujibu wa Katiba
ya Iamhuri
ya Muungano wa Tanzania, hawaruhusiwi kuwa
wanachama wa chama choehote
eha siasa wala
kujihusisha na shughuli
zozote
za kisiasa isipokuwa kupiga kura tu. Watumishi
hao ni:-
3.3.1 Askari wa Ieshi la Wanachi
wa Tanzania (JWTZ) na Ieshi la Kujenga Taifa (JKT), Polisi
na Magereza (kwa mujibu wa Ibara ya 147(3) na (4) ya Katiba
ya Iamhuri ya Muungano
wa Tanzania).
3.3.2 Majaji na Mahakimu
wa ngazi zote
(kwa mujibu wa Ibara ya 1l3A) ya Katiba
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanza-
nia).
3.3.3 Wajumbe na Watumishi wa Tume ya Uchaguzi
na
Wasima- mizi wa Uehaguzi (kwamujibu wa Ibara ya 74(14)na(l5)
ya Katiba ya Iamhuri ya Muungano wa Tanzania).
3
3.4 Mbali ya makundi yaliyoorodheshwa katika Katiba
kutoshiriki katika siasa yapo makundi mengine ambayo
kwa mujibu wa kazi
zao hayapaswi kushiriki katika siasa, lakini
hayakutajwa katika
Waraka wa Mkuu wa Utumishi wa Umma Na.1 wa Mwaka 1992,
mathalani, watumishi wa Idara ya U salama wa Taifa, Taasisi
ya Kuzuia Rushwa, Msajili wa Vyama vya Siasa, watumishi wa Ofisi ya Bunge,
na
Mawakili wa Serikali.
Mwaka 2013, Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema alipiga picha na mtu aliyevalia sare ya JWTZ katika mkutano wa hadhara na ikawa kesi kubwa mtaani. Basi sheria na iwe msumeno.
@LUMULINEWS.BLOGSPOT.COM
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni