Lebo

Ijumaa, 12 Juni 2015

Mjue Mtanzania aliyebuni kifaa cha kutatua tatizo la uhaba wa walimu

Ombeni Sanga

Watu wanaposema Tanzania ina vipaji siyo vya kucheza viduku tu, kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa katika gazeti la Mwananchi la leo, kuna taarifa kuhusu kijana Ombeni Sanga aliyebuni kifaa maalumu cha kutatua tatizo la upungufu wa walimu Tanzania. Taarifa kamili iko hapa:

Alipojiunga na Shule ya Sekondari ya Lumuli iliyopo  mkoani Iringa,   Ombeni Sanga alikuwa na matarajio makubwa ya kusoma masomo ya sayansi, ili baadaye aje kuwa mvumbuzi.
Kinyume na matarajio yake, hakuweza kupata kile alichokitarajia, kwani alikumbana na uhaba wa walimu wa sayansi shuleni hapo jambo lililomfanya akate tamaa ya kuendelea na masomo.

“Niliamua kukatisha masomo   nikiwa kidato cha pili kwa sababu tulikuwa hatusomi masomo ya sayansi. Nia yangu ilikuwa kuhamia shule nyingine lakini nikakosa kwa sababu sikuwa na fedha,” anasema

Changamoto hizo zilimpa Sanga fursa ya kuwa mbunifu na akaamua  kuunda chombo alichokibatiza jina la ‘ Boxpedia’ ambacho kitatumiwa na  wanafunzi  kujisomea mada mbalimbali za kitaaluma hata wakiwa nyumbani.

 “Hiki kifaa kitatumiwa na wanafunzi popote pale, kitakuwa na sauti za walimu ambao wanazichambua mada mbalimbali za masomo yote kwa ufasaha,” anasema.

Sanga anaeleza kuwa   lengo kubwa la kuunda boksi hilo ni kupambana na na uhaba wa  walimu wa masomo ya sayansi. Kwake ubunifu huo ni mbadala  utakaowarahisishia kazi wanafunzi.

 

Hata hivyo, anasema kasha hilo halitakuwa na sauti za walimu wa masomo ya sayansi tu bali hata masomo  ya sanaa na biashara, hivyo mwanafunzi atakuwa na  uwezo wa kuchagua mada aitakayo.











“Ni nyepesi kutumia  na haina ugumu kwa sababu mwanafunzi  ana kazi ya kusikiliza tu na akitaka anaweza kuchukua taarifa muhimu kwa ajili ya kujielewesha kwa kina mwenyewe,” anasema .

 Linafanyaje kazi?

Sanga anasema boksi hilo hurekodi sauti za walimu mahiri wa masomo yote katika mada zote.

‘’Mtumiaji wa boxpedia hubonyeza ‘code’ ya mada anayoitaka na kuanza kusikia sauti ya mwalimu wa mada katika somo kama  Baiolojia, Fizikia, historia,  Jiografia au lugha,’’ anaeleza.

Anasema sauti za walimu hao zitahaririwa kwanza kabla ya kuingizwa katika boksi hilo, kwa ajili ya matumizi na baada ya hapo ‘code’ za kuchagua mada zitatengenezwa.

    





 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni