Lebo

Jumapili, 14 Juni 2015

Profesa Lipumba amechukua fomu ya kugombea urais na kuahidi neema

Prof.Ibrahimu Lipumba

Mwenyekiti wa chama cha wananchi-CUF ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ametangaza nia rasmi na kuchukua fomu ya kugombea urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa mara ya tano mfululizo.

Pamoja na mambo mengine, mambo makubwa aliyoyazungumza Profesa Lipumba ni haya hapa:

Nachukua fomu kwa mara ya tano kwa sababu;

1. Kuhakikisha tunapata Katiba mpya.
Hili jina la (UKAWA)Umoja wa Katiba ya Wananchi mimi ndo nlilibuni. UKAWA ni ummoja wa vyama vilivyo sajiliwa.

2.Nina uwezo na nia ya kuwaondosha hawa mafisadi ambao badala ya kua jela wanachukua fomu ya kugombea urais wa CCM. Wanahitajika kuwa jela na mali zao zirejeshwe

Kidato cha tano nilisoma masomo ya hesabu uchumi na Geografia. Na chuo niliweka rekodi ya kufaulu Vizuri ambapo chuo kiliniomba nibakie shuleni nafundisha.

Nilienda Marekani kusoma na Kurudi kufundisha chuo kikuu cha Dar. Nilikua mshauri wa Mwinyi katika maswala ya Uchumi

Nilichaguliwa kuwa mshauri wa katibu mkuu wa Umoja wa mataifa katika maswala ya uchumi.

Bunge la marekani walinikaribisha niwafunde kwanini nataka madeni ya Afrika yafutwe.

Bunge la Marekani lilinikaribisha kuwashauri kuhusu mahusiano kati ya shirika la fedha na Afrika. Ushauri ulikubaliwa. Nimefanya ushauri wa Wizara ya fedha Namibia, Swaziland, Uganda. Katika maswala ya Ushauri nmefanya kwa muda mrefu.

Unapozungumzia maswala ya Uchumi nayaelewa sana.

Umasikini wa Tanzania unasababishwa na Siasa mbovu za Seikali ya CCM.

Niliulizwa umeoa? Ninaye mmoja ambaye anafanya kazi Umoja wa Mataifa ambapo yeye haruhusiwi kufanya shughuli za Kisiasa. Hata hivyo mimi ndo nagombea urais sio familia ndio inayogombea. Kama anataka siasa aingie kwa uwezo wake siyo aingie kwenye ubawa wa mume au mke.

Tunahitaji wakina mama waingie kwenye siasa kwa uwezo wao sio kwa kofia za familia kama ngazi. Hata Nyerere kwenye shughuli kubwa ulikua humuoni Mama Maria. Lakini sasa hivi wanabeba na familia zao.

3. Nataka wakina mama na Watoto wapate lisha bora na huduma za Msingi za Uzazi kwa kila Mtanzania. Watoto wanazaa wakiwa watoto, watoto wamedumaa, watoto wapewe Fursa za kusoma. Jambo la kuwekeza kwa watoto ndilo la msingi Imara

4. Kumaliza tatizo la ajira. Jiografia yetu ni nzuri ambayo ninzuri katika kujenga ajira. Mtwara kuna badari asilia ya kina kirefu. Hapo kuna fursa ya Biashara kwani kuna gesi, Tanga kuna bandari na kunakubali kila aina ya mazao. Vilevile sekta ya kilimo ni sehemu nzuri sana ya kutengeneza ajira.

Ujenzi wa miundo mbinu imara, sio tu tunaongeza ajira bali usalama pia kwani nchi nane tulizopakana nazo zinategemea bandari za Tanzania.

5. Hali ya Afya.
Tunatakiwa tuwe na hifadhi ya jamii kwani wazee wanateseka kwa kuwa hakuna huduma.

6. Ufisadi.
Kama nikichaguliwa kupeperusha bendera ya UKAWA, sitakuwa na huruma na mafisadi

Kama UKAWA watanipendekeza kupeperusha bendera, Nikiwa rais nitaunda Serikali ya Umoja wa kitaifa kupambana na ufisadi.

Nipo tayari Kumuunga mkono na Kumpigia debe Mgombea yoyote ambaye atapitishwa ndani ya UKAWA
. Ninacho waomba wananchi, Nendeni kujiandikisha ili tupige kura na kulinda kura pia, kwani miaka ya kuchakachuliwa imeshapitwa na wakati. Asanteni sana.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni