KATIBU MKUU WA CCM |
![]() |
MHE.PIUS MSEKWA |
Akizungumza na kituo cha redio cha East Africa Redio mapema leo asubuhi, Mhe.Msekwa amesema wananchi wamepoteza imani kwa chama hicho kutokana na kugubikwa na kashfa nyingi za ufisadi mkubwa unaorudisha nyuma maendeleo ya taifa huku viongozi wa chama hicho wakishindwa kuwawajibisha wahusika kiasi cha kuwafanya wananchi waamini kwamba chama kinasimamia misingi ya haki na maadili kwa viongozi.
Kashfa ya Richmond ndiyo iliyomwondoa Mhe.Edward Lowassa katika nafasi ya uwaziri mkuu kutokana na kutajwa moja kwa moja kuwa alihusika katika mchakato wa utoaji tenda kwa kampuni hewa ya kufua umeme yaani RICHMOND na kuligharimu taifa hasara ya mamilioni ya shilingi.
Mdadisi wa Masuala ya kisiasa ambaye pia ni mtaalamu wa masuala ya siasa na mahusiano ya kimataifa, Mtaalamu John Nzali anachambua kwamba endapo CCM wasipobadilika katika namna ya kuichukulia gadhabu ya umma dhidi ya ufisadi katika taifa huenda itaporomoka zaidi katika uchaguzi mkuu ujao. Amesema, "Kama CCM watashinda basi ni kwa asilimia si zaidi ya 60 endapo hawatafanya mabadiliko ya namna ya kushughulikia ufisadi, mipango kama KUJIVUA GAMBA haijawa na matokeo chanya mbele ya umma haswa baada ya kuongezeka kwa kashfa nyingine kama vile Tegeta Esrow. Kwa kifupi endapo wapiga kura wataendeleza kadhia ya kuchukia ufisadi na kutumia kura kama fimbo, hii inamaanisha kwamba CCM wanaweza kushuka kwa asilimia nyingine 30 kutoka kwenye 60% za mwaka 2010 endapo UKAWA watamuweka mgombea anaekubalika kwa wananchi vinginevyo mwenyekiti wa chama lazima achukue maamuzi magumu katika kumpata mgombea mwaka huu.
Mwenyekiti wa CCM, Mhe.Rais Jakaya Mrisho Kikwete |
Chama Cha Mapinduzi kinatarajiwa kumpitisha mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho siku chache mbeleni huku kukiwa na ushindani mkali baina ya watangaza nia zaidi ya 40 waliochukuwa fomu za kuomba ridhaa akiwemo mgombea wa darasa la saba kutoka kigoma aliyepewa fomu na CCM licha ya katiba ya nchi kutaja wazi kuwa mgombea kwa nafasi ya urais walau awe na shahada moja.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni